Wednesday, June 26, 2013

USHINDI DHIDI YA URUGUAY UTAWAUNGANISHA WABRAZIL - SCOLARI.

KOCHA wa timu ya taifa ya Brazil, Luis Felipe Scolari ameuelezea mchezo wa nusu fainali wa Kombe la Shirikisho dhidi ya Uruguay kama mchezo muhimu huku akidai kuwa ushindi watakaopata huko Belo Horizonte utasaidia kuwaunganisha wananchi wa taifa hilo. Waandamanaji zaidi ya 100,000 wanatarajiwa kuandamana karibu na maeneo ya Uwanja wa Estadio Mineirao kabla ya mechi ya Jumatano lakini Shirikisho la Soka Duniani-FIFA limedai kuwa wana uhakika kwamba kutakuwa na ulinzi wa kutosha kupelekea mchezo huo kuchezwa kama ulivyopangwa. Scolari amesema mchezo huo ni muhimu timu yao lakini wanahitaji kupiga hatua moja zaidi kwa kuifunga Uruguay ili waweze kufika fainali kwasababu mashabiki wa soka wa nchi hiyo wamekuwa pamoja nao kwa kipindi chote. Kocha aliongeza kuwa wananchi wa taifa wanatakiwa kutafuta jinsi ya kufanya kazi pamoja na sio kupigana wenyewe kwa wenyewe, labda katika miaka mitano au kumi wanaweza kuwa wamepiga hatua kubwa ya kimaendelea.

No comments:

Post a Comment