Thursday, June 27, 2013

WEBBER AAMUA KUACHANA NA LANGALANGA MWISHONI MWA MSIMU.

DEREVA nyota wa langalanga wa timu ya Red Bull, Mark Webber ameamua kuachana na mashindano hayo ikifikapo mwishoni mwa msimu huu. Katika miaka 12 ambayo amekuwa akishiriki michuano ya langalanga Webber ambaye pia amewahi kuendesha katika timu za Minard, Jaguar na Williams ameshinda mashindano mbalimbali ya Grand Prix mara tisa na kumaliza katika nafasi ya tatu katika mashindano ya dunia mara tatu. Akihojiwa kuhusiana na uamuzi huo Webber amedai kuwa anadhani huo ni wakati muafaka kwake kuachana na mbio za langalanga na kuangalia mambo mengine. Msimu wake mzuri ulikuwa ni mwaka 2010 ambapo aliongoza karibu msimu wote kabla ya kuteleleza katika mashindano matatu ya mwisho na kushuhudia dereva mwenzake wa Red Bull Sebastian Vettel na Fernando Alonso wa Ferrari wakimpita. Dereva wa Lotus Kim Raikkonen ambaye ni bingwa wa michuano ya dunia mwaka 2007 ndio anapewa nafasi kubwa kuchukua nafasi ya Webber ambaye aliingia katika langalanga mwaka 2002.


No comments:

Post a Comment