Friday, June 28, 2013

UNITED YATAKA KUIBOMOA EVERTON TENA.

KLABU ya Manchester United imeamua kumtengea kitita cha paundi milioni 15 kwa ajili ya kumnasa beki wa Everton, Leighton Baines. Baada ya kukataa ofa ya awali ya United ya Pauni Milioni 12, Everton imesisitiza kuwa beki huyo wa kushoto wa kimataifa wa England hauzwi. Lakini United imepania kupanda dau hadi paundi milioni 20 katika kuwania saini ya mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 28. Mrithi wa Moyes, Everton, Roberto Martinez anataka kumbakzia beki huyo na klabu hiyo inataka kumpa mkataba mpya ikimuongezea mshahara hadi paundi 70,000 kwa wiki. Mpango huu unamuweka shakani beki Mfaransa, Patrice Evra juu ya mustakabali wake Old Trafford na wazi sasa anaweza kuhamia Monaco au Paris Saint-Germain. 




No comments:

Post a Comment