Friday, June 28, 2013

FENERBAHCE KUKATA RUFANI KUPINGA ADHABU YAO.

MWENYEKITI wa klabu ya Fenerbahce ya Uturuki kwa mara nyingine amekana tuhuma za kupanga matokeo zinazoikabili klabu hiyo na kudai kuwa ana uhakika rufani yao walioiwasilisha Shirikisho la Soka barani Ulaya-UEFA itabadilisha uamuzi wa kuwafungia kushiriki michuano ya Ligi ya Mabingwa barani humo. Mwenyekiti huyo aitwaye Aziz Yildirim amesema Fenerbahce itatoa ndege kwa ajili ya watu watakaopeleka ushahidi wa kuitetea klabu hiyo katika usikilizwaji wa rufani yao. Fenerbahce walifungiwa mapema wiki hii kutoshiriki michuano yoyote inayoandaliwa na UEFA ambayo watafuzu kucheza kuwanzia msimu ujao kutokana na kukutwa na hatia ya kupanga matokeo katika mechi za Ligi Kuu nchini Uturuki mwaka 2011. Yildirim ambaye alihukumiwa mwaka jana kwa makosa ya jinai ambapo amekata rufani katika mahakama ya juu nchini humo, amedai kuwa klabu hiyo ni safi na hawajajihusisha na suala hilo wanalotuhumiwa nalo. Klabu hiyo imemaliza katika nafasi ya pili kwenye ligi kuu ya nchi hiyo na wamefuzu kushiriki Ligi ya Mabingwa Ulaya ambapo wataanzia hatua ya mtoano kabla ya kuingia kwenye hatua ya makundi ya timu 32.

No comments:

Post a Comment