Friday, June 28, 2013

WAKANYAGANA KUMUONA MESSI SENEGAL.

MSHAMBULIAJI wa kimataifa wa Argentina Lionel Messi ametua nchini Senegal jana kwa ndege binafsi na kulakiwa katika Uwanja wa Ndege wa Dakar na mashabiki wa soka na vijana wadogo waliotoka pembe mbalimbali za nchi hiyo. Nyota huyo anayecheza katika klabu ya Barcelona alialikwa na shule ya soka ya Qatar Aspire ambao wana tawi lao nchini humo kwa ajili ya kwenda kwenye kampeni ya kupiga vita ugonjwa wa malaria. Kwa mujibu wa waratibu ya ziara hiyo maelfu ya neti ambazo zitakuwa na picha ya Messi zitasambazwa kwa watoto na familia katika vijiji mbalimbali nchini humo. Messi atasafiri kwa helikopta kwenda Saly eneo la karibu na mji wa Dakar ambapo atatembelea nyumba za yatima na kuongea na wenyeji wa hapo jinsi watakavyoweza kujikinga na malaria.

No comments:

Post a Comment