Friday, June 28, 2013

TUNA UWEZZO WA KUPAMBANA NA WALIO BORA - PRANDELLI.

KOCHA wa timu ya taifa ya Italia Cesare Prandelli amesema kikosi chake kina uwezo wa kupambana na timu bora kufuatia kuenguliwa kwa changamoto ya mikwaju ya penati 7-6 katika mchezo wa nusu fainali ya Kombe la Mabara. Italia jana usiku walifanikiwa kuing’ang’ania Hispania inayonolewa na Vicente del Bosque kwenda sare ya bila kwa bila katika dakika tisini za kawaida na baadae kuongezewa dakika zingine ambazo nazo hazikuzalisha mabao na kupelekea mchezo huo kuamuliwa kwa matuta. Prandelli amesema wametolewa katika michuano hiyo kwa heshima na kuonyesha uma kuwa wanaweza kushundani na timu bora kabisa duniani. Italia walifanikiwa kuwabana wapinzani wao na kushindwa kupiga mpira wowote uliolenga goli katika kipindi cha kwanza na Prandelli amewasifu wachezaji wake ka kucheza kwa nidhamu ya hali ya juu na kutoruhusu makosa ambayo yangewagharimu. Pamoja na kucheza vyema na timu bora kabisa duniani Prandelli hakuwa tayari kuzungumzia mikakati yake katika michuano ya Kombe la Dunia mwakani akidai kuwa muda bado haujafika kwakuwa bado hawajafuzu kucheza michuano hiyo.

No comments:

Post a Comment