Sunday, June 30, 2013

HADHI YA FIFA IMEIMARIKA - BLATTER

RAIS wa Shirikisho la Soka Duniani-FIFA, Sepp Blatter amedai kuwa hadhi ya shirikisho hilo imeimarika kutokana na fainali za michuano ya Kombe la Shirikisho inayoendelea nchini Brazil licha ya maandamano yanayoendelea nchini humo. Akiongea kwa mara ya kwanza, tangu maandamano hayo kuanza, Blatter amesema anawahurumia raia wa nchi hiyo wanaoandamana katika miji mia moja nchini Brazil. Maandamano zaidi yanategemewa kuwepo kabla ya fainali yamichuano hiyo kati ya Brazil na Hispania katika Uwanja wa Maracana uliopo jijini Rio de Janeiro na kuna wasiwasi mkubwa kuwa huenda rais wa nchi hiyo Dilma Rousseff huenda asihudhurie fainali hiyo. Blatter amesema FIFA imekuwa na nguvu zaidi na hadhi yake imeimarishwa huku mchezo wa soka umekuwa na nafasi kubwa miongoni mwa watu wa Brazil na imewapa fursa ya kuelelezea hisia zao. Blatter amesema anawahurumia sana raia wa nchi hiyo kwa kuwa anafahamu masuala wanayoyapinga kupitia maandamano hayo ya amani na ameongea kuwa anatarajiwa serikali ya nchi hiyo itatatua masuala hayo kabla ya kuanza kwa fainali ya Kombe la Dunia itakayoandaliwa nchini humo mwaka ujao.

No comments:

Post a Comment