Sunday, June 30, 2013

NEYMAR, INIESTA, PIRLO, SUAREZ, RAMOS NA PAULINHO KUCHUANA TUZO YA MCHEZAJI BORA MICHUANO YA KOMBE LA SHIRIKISHO.

SHIRIKISHO la Soka Duniani-FIFA limetangaza orodha ya wachezaji sita watakaogombea tuzo ya mchezaji bora wa michuano ya Kombe la Shirikisho ambao ni Neymar, Andres Iniesta, Andrea Pirlo, Luis Suarez, Sergio Ramos na Paulinho. Majina hayo yamechaguliwa na kamati maalumu ya ufundi ya FIFA na mshindi atatambulishwa mbele ya waandishi wa habari baada ya mchezo wa fainali utakaochezwa baadae leo. Wachezaji wanne kati hao wanatarajiwa kuwemo katika vikosi vya nchi zao katika mchezo wa fainali kati ya wenyeji Brazil na Hispania katika Uwanja wa Maracana jijini Rio de Janeiro. Neymar amefunga mabao matatu kwa timu yake ya Brazil na ni mchezaji pekee kushinda tuzo ya mchezaji bora wa mechi mara mbili katika michuano hiyo huku mbrazil mwenzake Paulinho akifunga mabao mawili katika mechi tatu.

No comments:

Post a Comment