Sunday, June 30, 2013

CHELSEA YATHIBITISHA KUWATEMA WANNE.

KLABU ya Chelsea imethibitisha kuwatema wachezaji wake Paulo Ferreira, Yossi Benayoun, Florent Malouda na Ross Turnbull baada ya mikataba yao kumalizika. Ferreira ameichezea klabu hiyo mechi 217 katika kipindi cha miaka tisa aliyokuwepo Stamford Bridge na kuisaidia kunyakuwa mataji matatu ya Ligi Kuu nchini Uingereza na moja la Ligi ya Mabingwa barani Ulaya walilochukua mwaka jana. Benayoun alitua Chelsea mwaka 2010 ili kuziba nafasi ya Joe Cole lakini alishinda kupata namba ya kudumu katika kikosi cha kwanza kutokana na kusumbuliwa na majeruhi ya mara kwa mara na kupelekwa kwa mkopo katika vilabu Arsenal na West Ham United katika vipindi tofauti. Malouda alichukuliwa kutoka mwaka mabingwa wa Ligi Kuu nchini Ufaransa mwaka 2007 klabu ya Olympique Lyon na kushinda vikombe kadhaa vya ligi na ligi ya mabingwa lakini alienguliwa ghafla katika kikosi cha kwanza cha timu hiyo msimu uliopita na kufanya mazoezi na wachezaji wa akiba wa timu hiyo. Turnbull alisajiliwa akitokea Middlesbrough mwaka 2009 kama golikipa wa akiba akimsaidia Petr Cech na kucheza mechi 19 pekee katika miaka minne ambayo amekuwepo katika klabu hiyo yenye maskani yake magharibi mwa jiji la London.

No comments:

Post a Comment