Sunday, June 30, 2013

WILLIAMS, DJOKOVIC WAENDELEA KUPASUA ANGA WIMBLEDON.

MWANADADA nyota wa mchezo wa tenisi kutoka Marekani, Serena Williams amefanikiwa kuingia katika mzunguko wan ne wa michuano ya Wimbledon baada ya kumuengua Kimiko Date-Krumm wa Japan katika mzunguko wa tatu wa michuano hiyo. Williams ambaye anashika namba moja katika orodha za ubora duniani na bingwa mtetezi wa michuano katika mchezo huo alimshinda Krumm kwa 6-2 6-0 akitumia muda wa dakika 61 pekee. Krumm mwenye umri wa miaka 42 amekuwa mwanamke mwenye umri mkubwa zaidi kuingia mzunguko wa tatu wa michuano hiyo inayoendelea jijini London, Uingereza. Kwa upande wanaume Novak Djokovic wa Serbia naye amefanikiwa kutinga hatua ya 16 bora baada ya kumtandika Jeremy Chardy wa Ufaransa kwa 6-3 6-2 6-2.

No comments:

Post a Comment