Sunday, June 30, 2013

VILLAS-BOAS KUSTAAFU MIAKA 10 IJAYO.

MENEJA wa klabu ya Tottenham Hotspurs, Andre Villas-Boas amebainisha mipango ya kustaafu kufundisha wakati atapofikisha miaka 45. Kocha huyo mwenye miaka 35 raia wa Ureno amekuwa kocha mdogo zaidi kushinda taji la Europa League wakati akiwa na klabu ya Porto miaka miwili iliyopita, kabla ya kwenda Chelsea ambako alitimuliwa kwa kushindwa kufanya vyema na kwenda Spurs alipo sasa. Pamoja na kwamba Villas-Boas amesisitiza kuwa anafurahia kazi hiyo ya ukocha lakini haoni kama atafanya shughuli hiyo kwa kipindi kirefu kama makocha wengine. Villas-Boas amesema amapenzi yake katika soka yanamfanya aishi maisha ya wasiwasi kwa kipindi cha miezi 11 katika mwaka na anadhani maisha yamruhusu mtu kufurahia vitu vingine zaidi ndio maana ameamua baada ya miaka 10 ijayo atastaafu rasmi shughuli hiyo. Kocha huyo aliendelea kudai kuwa amekuwa na ndoto za kipindi kirefu kushiriki mashindano ya Dakar Rally hivyo akiachana na mambo ya ukocha ataelekeza shughuli zake katika mashindano hayo yenye historia ya kipekee duniani. 


No comments:

Post a Comment