Tuesday, July 23, 2013

FINIDI GEORGE KUVIFUNDISHA VITOTO VYA REAL MALLORCA.

MCHEZAJI wa zamani wa kimataifa wa Nigeria, Finidi George ametajwa kuwa kocha mpya wa timu ya vijana chini ya umri wa miaka 16 ya Real Mallorca ya Hispania. Akihojiwa na mtandao wa Supersport, George amesema ni heshima kubwa kwake kupata nafasi hiyo na ni mategemeo yake wataweza kuwapandisha wachezaji watatu au wanne katika kikosi cha kwanza cha timu hiyo. George amesema kwasasa ana leseni ya daraja la B ya ukocha inayotambuliwa na Shirikisho la Soka barani Ulaya-UEFA lakini kutokana na kazi hiyo aliyopata itakuwa kazi rahisi kwake kusomea kozi ya ukocha mwakani ili aweze kupata leseni daraja A. Mchezaji huyo ambaye alikuwa sehemu ya kikosi cha timu ya Ajax Amsterdam ya Uholanzi ambacho kilinyakuwa taji la Ligi ya Mabingwa barani Ulaya amesema jina zuri alilojitengenezea kipindi akicheza soka ndio linamemfanya kupata nafasi hiyo. Amesema anawakumbuka wachezaji wenzake wengi aliocheza nao wakati akiwa Ajax, Malorca na Real Betis ambao kwasasa ni makocha hivyo akifanya kazi hiyo kwa kujituma anadhani na yeye atakuwa katika nafasi kama za wenzake huko mbele.

No comments:

Post a Comment