Tuesday, July 23, 2013

MADRID YAMKOMALIA VILLAS-BOAS.

MENEJA wa klabu ya Tottenham Hotspurs, Andre Villas-Boas kwa mara nyingine amesisitiza kuwa Gareth Bale hawezi kwenda popote katika kipindi hiki cha usajili wa majira ya kiangazi lakini gazeti la Marca la Hispania limedai kuwa tayari nyota huyo wa kimataifa wa Wales ameshakamilisha uhamisho kwenda Real Madrid. Gazeti hilo lilidai kuwa Madrid wako katika hatua za mwisho za kumsainisha Bale mkataba wa miaka sita ambao utakuwa na thamani ya paundi milioni 8.5 kwa mwaka. Mbali na taarifa hiyo gazeti hilo pia lilidai kuwa Bale tayari amewaambia viongozi wa Spurs kuwa anataka kuondoka kwenda Santiago Bernabeu. Akihojiwa katika ziara ya Spurs nchini Hong Kong, Villas-Boas kwa mara nyingine tena alikana tetesi hizo na kudai kuwa Bale haendi kokote lakini akithibitisha kuwa klabu hiyo ina mpango wa kumsajili mshambuliaji wa Valencia Roberto Soldado.

No comments:

Post a Comment