Wednesday, July 24, 2013

HAYATOU AMTEUA JORDAAN KUWA MSHAURI WAKE.

OFISA mkuu wa zamani wa kamati ya maandalizi ya michuano ya Kombe la Dunia 2010, Dr Danny Jordaan ameteuliwa kuwa mshauri wa rais wa Shirikisho la Soka barani Afrika-CAF Issa Hayatou. Katika taarifa iliyotumwa katika mtandao wa CAF imeeleza kuwa uteuzi wa Jordaan umekuja kufuatia mchango wake anaoendelea kutoka katika kunyanyua soka la Afrika. huku Hayatou akiongeza kuwa anategemea mafanikio makubwa kwa kushirikiana vyema na Jordaan. Jordaan amewahi kufanya kazi kama Ofisa Mkuu wa Chama cha Soka cha Afrika Kusini-SAFA kati ya mwaka 1997 na 2001 na pia amefanya kazi kama mjumbe wa bodi ya masoko na luninga ya FIFA kati ya mwaka 1998 na 2003. Kwasasa Jordaan anafanya kazi kama mshauri maalumu wa FIFA wa michuano ya Kombe la Dunia 2014 itakayofanyika nchini Brazil.

No comments:

Post a Comment