Wednesday, July 24, 2013

MARTINO ATAPATA MAFANIKIO BARCELONA - CRUYFF.

NGULI wa soka wa zamani wa klabu ya Barcelona, Yohan Cruyff anaamini kuwa kocha mpya wa klabu hiyo Gerardo Martino anaweza kupata mafanikio kama ilivyokuwa kwa Frank Rijkaard na pep Guardiola pamoja nauzoefu mdogo alionao katika soka la Ulaya. Rijkaard alifanikiwa kushinda mataji matano kati ya kipindi cha mwaka 2003 na 2006 pamoja na kutoka kufundisha klabu ndogo ya Sparta Rotterdam wakati Guardiola ambaye alirithi mikoba yake yeye aliibuka kukota kikosi B cha klabu hiyo lakini naye alipata mafanikio makubwa. Barcelona walitangaza kumpa mkataba wa miaka miwili Martino huku akiwa hajafundisha timu yoyote barani Ulaya lakini Cruyff anaamini kocha mwenye umri wa miaka 50 ataleta mafanikio Camp Nou. Cruyff amesema hajui chochote kuhusu kocha huyo lakini Rijkaard na Guardiola walianza kuifundisha Barcelona wakiwa hawana mafanikio yoyote kama makocha hivyo hana shaka kwamba Martino naye anaweza kufanikiwa.

No comments:

Post a Comment