Wednesday, July 24, 2013

MARADONA AFANYIWA UPASUAJI WA MACHO.

NGULI wa soka nchini Argentina, Diego Maradona amefanyiwa upasuaji wa macho ambao umemalizika kwa mafanikio. Maradona mwenye umri wa miaka 52 alifanyiwa upasuaji huo ili kukwangua utandu uliokuwa katika macho yake ambao ulikuwa ukisumbua kutokuona sawasawa katika mji wa Mendoza uliopo magharibi mwa Argentina. Daktari aliyemfanyia upasuaji Roberto Zaldivar aliwaambia waandishi wa habari kuwa Maradona alikuwa akiendelea vyema na upasuaji huo ni wa kawaida kwa watu wenye umri kama wake. Maradona anatarajiwa kufanyiwa uchunguzi kabla ya kurejea Buenos Aires na baadae kwenda Dubai ambako anafanya kazi kama balozi wa soka.

No comments:

Post a Comment