Tuesday, July 23, 2013

MARTINO KOCHA MPYA BARCELONA.

KLABU ya Barcelona imemteua Gerardo Martino kutoka Argentina kuwa kocha mpya wa klabu hiyo akichukua nafasi ya Tito Vilanova aliyejiuzulu kutokana na maradhi ya saratani yanayomsumbua. Martino mwenye umri wa miaka 50 amekubali kusaini mkataba wa miaka miwili wa kuwafundisha Barcelona ambao ni mabingwa wa La Liga msimu uliopita. Makubaliano hayo yalifanyika mapema jana ambapo wasaidizi wake wanatarajiwa kuwa waargentina wenzake Elvio Paolorroso na Jorge Pautasso ambao alikuwa akifanya nao kazi katika klabu ya Newell Old Boys ya Argentina. Martino hajawahi kufundisha Ulaya kabla lakini amefundisha vilabu mbalimbali nchini Argentina ikiwemo timu ya taifa ya Paraguay na pia ni rafiki wa karibu wa nyota wa Barcelona Lionel Messi na baba yake Jorge kwasababu wanatoka katika mji mmoja wa Rosario. Kocha huyo anatarajiwa kutua nchini Hispania Jumatano kwa ajili ya kutambulishwa mbele ya waandishi wa habari na mashabiki kabla ya kuanza kibarua chake rasmi Alhamisi ya wiki hii.

No comments:

Post a Comment