Tuesday, July 23, 2013

GUARDIOLA USO KWA USO NA BARCELONA.

MENEJA mpya wa klabu ya Bayerm Munich, Pep Guardiola anatarajiwa kukutana na timu yake ya zamani ya Barcelona katika mchezo wa kirafiki kwa ajili ya kujiandaa na msimu mpya wa ligi barani Ulaya. Barcelona walitua jijini Munich bila kuwa na kocha wao mkuu baada ya Tito Vilanova kujiuzulu wadhifa wake Ijumaa iliyopita kwa matatizo ya kiafya huku klabu hiyo ikiwa katika mchakato wa kutafuta kocha mpya. Msadizi wa Vilanova Jordi Roura ndiye atachukua mikoba yake kwa muda katika mchezo huo wa kirafiki utakaofanyika Allianz Arena. Guardiola alichukua mikoba rasmi ya kuinoa Bayern mapema mwezi uliopita baada ya kuchukua mapumziko ya mwaka mzima toka alipoondoka Barcelona katika kipindi cha majira ya kiangazi mwaka jana.

No comments:

Post a Comment