Tuesday, July 23, 2013

FIFA YAITOLEA KITANZI CAMEROON.

SHIRIKISHO la Soka Duniani-FIFA limetangaza kuondoa adhabu ya kuifungia Cameroon kushiriki mechi za kimataifa baada ya kuundwa kamati ya muda itakayoongozwa na Joseph Owona. Kwa maana hiyo klabu ya Coton Sport sasa inaweza kucheza na Sewe katika michuano ya Kombe la Shirikisho mwishoni mwa wiki hii huku pia timu ya taifa ya Cameroon nayo ikichuana na Cameroon katika mechi za kufuzu michuano ya Mataifa ya Afrika kwa wachezaji wa ndani-CHAN. FIFA ilifikia hatua ya kulifungia Shirikisho la Soka la Cameroon-Fecafoot baada ya kutokea mganganyiko katika uchaguzi wake ambao ulimrudisha madarakani Mohamed Iya ambaye alikuwa akikabiliwa na kesi mahakamani ya matumizi mabaya ya fedha wakati akiwa kiongozi wa kampuni moja ya katani nchini humo. Katika barua iliyotumwa na FIFA katika mtandao wake imedai kuwa wamefikia uamuzi huo baada ya kuundwa kwa kamati hiyo itakayoliongoza shirikisho hilo kwa muda mpaka hapo utakapofanyika uchaguzi mwingine.

No comments:

Post a Comment