Tuesday, July 23, 2013

NFF YAWAFUNGIA MAISHA WACHEZAJI NA VIONGOZI.

SHIRIKISHO la Soka nchini Nigeria-NFF limewafungia maisha wachezaji na viongozi wote walioshiriki katika mechi mbili za mtoano kwa ajili ya kupanda daraja. Katika mechi hizo klabu ya Plateau United Feeders waliifunga Akurba FC kwa mabao 79-0 wakati timu ya Police Machine FC wenyewe waliigaragaza Bubayaro FC kwa mabao 67-0. Mbali na adhabu hizo kwa wachezaji na viongozi vilabu navyo vimefungiwa miaka 10 huku kamati ya NFF iliyokuwa ikichunguza tukio hilo imependekeza waamuzi nao wafungiwe maisha kujishughulisha na mambo ya michezo. Plateau United Feeders na Police Machine zilikwenda kwenye mechi zikiwa na alama sawa huku kila timu ikitaka kupanda daraja ambapo mabao 72 ya Feeders yalifungwa katika kipindi cha pili wakati Police Machine nao walifunga mabao 61 baada ya kipindi cha mapumziko. Matokeo hayo yalizua gumzo kubwa na kupelekea NFF kuanza uchunguzi haraka huku Shirikisho la Soka Duniani-FIFA nalo likifuatilia tukio hilo kujua hatma yake.

No comments:

Post a Comment