Wednesday, July 31, 2013

NDOTO ZANGU ZIMETIMIA - NEYMAR.

MSHAMBULIAJI mpya wa klabu ya Barcelona, Neymar amebainisha kuwa anamhusudu Lionel Messi na kudai kuwa kucheza naye katika timu moja ni kama ndoto ambazo zimekuja kuwa kweli. Nyota wa kimataifa wa Brazil alicheza mechi yake ya kwanza akiwa na klabu hiyo katika mchezo wa kirafiki dhidi ya timu ya Lechia Gdansk akiingia dakika 15 za mwisho kuchukua nafasi ya Alexis Sanchez. Akihojiwa mara baada ya mchezo huo, Neymar alikiri kuwa ndoto zake alizokuwa nazo katika kipindi kirefu zimeanza kuwa kweli baada ya kucheza mechi hiyo ya kwanza. Nyota mwenye miaka 21 anatarajiwa kukutana na klabu yake ya zamani ya Santos katika mechi ya kirafiki Agosti 2 mwaka huu.

No comments:

Post a Comment