Wednesday, July 31, 2013

HENRY AKABIDHIWA UNAHODHA KIKOSI CHA WACHEZAJI NYOTA WA LIGI YA MAREKANI.

MSHAMBULIAJI wa zamani wa Ufaransa, Thierry Henry ameteuliwa kuwa nahodha wa kikosi cha wachezaji nyota wa Ligi Kuu nchini Marekani-MLS kwa ajili ya mechi yao ya kirafiki dhidi ya AS Roma itakayofanyika jijini Kansas. Henry alikabidhiwa unahodha na kocha wa kikosi hicho Peter Vermes na kufuata nyayo za David Beckham ambaye aliwahi kuwa nahidha wa kikosi hicho katika mechi ya kirafiki dhidi ya Manchester United miaka miwili iliyopita. Henry ndio ilikuwa mara yake ya kwanza kucheza katika kikosi cha wachezaji nyota wa MLS ambapo United ilishinda kwa mabao 4-0 lakini mwaka mmoja baadae alikisaidia kikosi hicho kuigaragaza Chelsea kwa mabao 3-2. Kwa Roma hiyo itakuwa mechi yao ya kwanza kati ya nne watakazocheza wakati wakiwa huko Amerika Kaskazini kwa ajili ya maandalizi msimu mpya wa Ligi Kuu ya Soka nchini Italia.

No comments:

Post a Comment