Wednesday, July 31, 2013

IAAF YAPANIA KUKOMESHA WANARIADHA KUTUMIA DAWA ZILIZOKATAZWA.

MAKAMUwa rais wa Shirikisho la Kimataifa la Riadha-IAAF, Sebastian Coe amedai kuwa shirikisho hilo limejipanga kukomesha matumizi ya dawa za kuongeza nguvu baada ya wanariadha wawili nyota wa mbio fupi kukutwa na hatia ya kutumia dawa hizo mapema mwezi huu. Kauli hiyo ya Coe ameitoa jijini Moscow mji ambao ndio utakuwa mwenyeji wa mashindano ya riadha ya dunia baadae mwezi ujao baada ya Tyson Gay wa Marekani na Asafa Powell wa Jamaica kushindwa katika vipimo vyao walivyofanyiwa. Coe amesema kitu cha msingi kuhakikisha wanawafanyia wanaraidha vipimo vya mara kwa mara ili kuhakikisha mashindano ya hayo ya dunia yanafanyika katika hali salama ya bila mwanariadha yoyote kukutwa na dawa hizo zilizopigwa marufuku. Coe alikiri kuwa litakuwa ni suala lisilowezekana kwake kudai kuwa itafikia muda matukio kama hayo kuisha katika michezo lakini hivi sasa wanafuatilia suala hilo kwa karibu zaidi kuliko ilivyokuwa hapo mwanzo. Mashindano ya raidha ya dunia yatakuwa ya kwanza makubwa kufanyika jijini Moscow toka mji huo ulioandaa michuano ya olimpiki mwaka 1980 na yatafanyika katika Uwanja wa Luzhniki ambao ndio zilizikofanyika sherehe za ufunguzi wa olimpiki mwaka huo.

No comments:

Post a Comment