Tuesday, July 30, 2013

PAPARAZI AMSHITAKI MARADONA KWA KUMPIGA.

MPIGA mmoja wa gazeti la watu maarufu nchini Argentina, amemtuhumu nguli wa soka wa zamani wa nchi hiyo Diego Maradona kwa kumpiga teke la kiuno na kumfungulia mashitaka polisi kutokana na tuhuma hizo. Mpiga picha huyo wa gazeti la Gente aitwaye Enrique Medina amesema shambulio hiyo lilitokea nje ya nyumba ya Maradona Jumapili usiku wakati akisubiria kumpiga picha nyota huyo. Medina alidai kuwa wakati akiwa hapo nguli huyo alimkimbilia kama anataka kupiga mpira wa adhabu na kumpiga kiunoni pamoja na kwenye paja na kumsababishia maumivu makali. Mwandishi huyo aliendelea kudai kuwa teke alilopigwa halikuwa la mtu wa kawaida kwani lilitoka kwa mtu ambaye amezoea kufanya hivyo na alionekana kuwa na hasira nyingi. Maradona amekuwa akilalamika mara kwa mara vyombo vya habari kumfuatilia kwa karibu ambapo mwaka 1994 aliwahi kufanya tukio kubwa kwa kupiga risasi hewani kuwatimua waandishi waliokuwa wakimfuatilia ambapo bunduki yake ilifungiwa miaka miwili.

No comments:

Post a Comment