Tuesday, July 30, 2013

BECKHAM AVAMIA KAMBI MADRID KUSALIMIA.

KIUNGO mahiri wa zamani wa klabu ya Real Madrid, David Beckham amevamia kambi ya timu hiyo iliyopo jijini Los Angeles, Marekani kwa ajili ya kusalimiana na wachezaji wenzake wa zamani aliowahi kucheza nao. Madrid ambao hivi sasa wananolewa na meneja mpya Carlo Ancelotti wapo huko kwa ajili ya maandalizi ya msimu mpya wa Ligi Kuu nchini Hispania unaotarajiwa kuanza kutimua vumbi Agosti 18 mwaka huu. Kabla ya kuitembelea Madrid, Beckham alitembelea klabu yake ya zamani ya Los Angeles Galaxy kabla pia ya kuzitembelea Phoenix, Miami na Saint Louis. Beckham alipiga picha na Cristiano Ronaldo baada ya mazoezi na pia kusaini fulana na mipira kwa mashabiki waliobahatika kwenda kuwatizama Madrid wakiwa mazoezini.

No comments:

Post a Comment