Tuesday, July 30, 2013

CAF YATUPILIA MBALI OMBI LA AL AHLY KUSOGEZA MECHI YAO DHIDI YA ORLANDO PIRATES.

SHIRIKISHO la Soka barani Afrika-CAF limetupilia mbali maombi ya Al Ahly waliotaka kusogeza mbele mchezo wao wa Ligi ya Mabingwa ya Afrika dhidi ya Orlando Pirates iliyotakiwa kuchezwa Agosti 4 kwa ajili ya mfungo wa Ramadhan. Katika taarifa ya klabu hiyo iliyotumwa katika mtandao wake walithibitisha kupokea barua kutoka CAF ya kukataliwa ombi lao hilo. Mapema Jumapili iliyopita mkurugenzi wa michezo wa Al Ahly Sayed Abdel Hafiz aliviambia vyombo vya habari nchini Misri kuwa klabu hiyo imeomba mchezo huo kusogezwa mbele kwa siku tano ili kuepuka matatizo wachezaji wake waliyokutana nayo katika mchezo dhidi ya Zamalek. Hafiz alidai kuwa wachezaji wake walikabiliwa na wakati mgumu katika mchezo huo baada ya kukataa kufungua na kucheza mchezo huo katika kipindi cha mchana kilichokuwa na joto kali. Klabu hiyo pia imetakiwa kutafuta uwanja mwingine kwa ajili ya mchezo huo wa kundi A baada ya jeshi kuwakatalia uwanja wao wa Air Defence uliopo jijini Cairo kwasababu za kiusalama.

No comments:

Post a Comment