Monday, July 29, 2013

BOLT KUSHINDANA NA FARAH KATIKA MBIO ZA HISANI.

MWANARIADHA nyota wa mbio fupi, Usain Bolt amekubali kushindana na nyota wa mbio ndefu kutoka Uingereza Mo Farah katika mbio za hisani za mita 600. Farah ambaye alishinda medali za dhahabu katika mbio za mita 5,000 na 10,000 katika mashindano ya olimpiki yaliyofanyika London mwaka jana ndio wanariadha waliong’aa katika michuano hiyo sambamba na Bolt ambaye naye alishinda dhahabu katika mbio za mita 100 na 200. Akihojiwa Bolt amesema atajiandaa kwa ajili ya mbio hizo ingawa alikiri zitakuwa ngumu kwake kwakuwa amezoea kukimbia umbali mfupi na kwa kasi kubwa. Bolt ambaye anashikilia rekodi ya dunia katika mbio za mita 100 na 200 alidai kuwa kukimbia mita 600 akijiandaa vizuri ataweza lakini mita 1,500 ni suala ambalo halitawezekana kwake.

No comments:

Post a Comment