Monday, July 29, 2013

REINA ASONONESHWA NA LIVERPOOL KUMPELEKA KWA MKOPO NAPOLI.

GOLIKIPA wa klabu ya Liverpool, Pepe Reina ameeleza kusikitishwa kwake kwa timu hiyo kukubali kumpeleka kwa mkopo katika klabu ya Napoli ya Italia kabla ya kumwambia kwanza. Golikipa huyo wa kimataifa wa Hispania, mwenye umri wa miaka 30 alijiunga na Italia kwa mkpo wa msimu mmoja baada ya Liverpool kumsajili Simon Mignolet kutoka Sunderland. Katika barua yake aliyowaandikia mashabiki wa klabu hiyo, Reina amesema alikuwa bado anataka kuendelea kubakia Anfield baada ya mipango yake ya kwenda Barcelona kukwama. Reina amesema ameshangazwa na hatua iliyochukuliwa na klabu hiyo kumtoa kwa mkopo bila hata kushauriana naye lakini amemua kuelewa kwasababu muda mwingine maamuzi magumu lazima yatolewe katika soka.

No comments:

Post a Comment