Monday, July 29, 2013

MIPANGO YA USAJILI IKO POA - MOYES.

MENEJA mpya wa klabu ya Manchester United, David Moyes amesisitiza kuwa mipango yake ya usajili katika kipindi hiki cha majira ya kiangazi inakwenda vizuri pamoja na kushindwa kufanya usajili mkubwa mpaka sasa. United mpaka sasa wametuma ofa mbili kwa ajili ya kujaribu kumsajili Cesc Fabregas lakini wamekataliwa na Barcelona huku wakipigwa bao na Bayern Munich kwa kushindwa kupata saini ya Thiago Alcantara. Akihojiwa kuhusu mipango yake ya usajili, Moyes amesema usajili wa Fabregas sio pekee ambao anautegemea kwa msimu huu kwani anategemea katika muda uliobakia wa usajili atakuwa amepata wachezaji kadhaa. Mbali na Fabregas United pia wamekuwa wakihusishwa kutaka kuwasajili Maouane Fellaini na kiungo wa kati Yohan Cabaye ambaye anategemewa kuziba pengo la Paul Scholes.

No comments:

Post a Comment