Monday, July 29, 2013

HAMILTON AIBUKA KIDEDEA MASHINDANO YA HUNGARY GRAND PRIX.

DEREVA nyota wa mashindano ya langalanga, Lewis Hamilton wa timu ya Marcedes amefanikiwa kupanda ushindi wake wa kwanza akiwa na timu hiyo baada ya kuibuka kidedea katika mashindano ya Grand Prix ya Hungary. Hamilton alijituliza na kutumia kasi akiwashinda dereva Kimi Raikkonen wa timu ya magari ya Lotus aliyemaliza wa pili na Sebastien Vettel wa Red Bull aliyemaliza wa tatu. Mark Webber wa Red Bull alionyesha umahiri wake kwa kujikwamua kutoka nafasi ya kumi alikoanzia mashindano hadi kumpiku dereva wa Ferrari, Fernando Alonso. Kutokana na hali hio Raikkonen sasa anapanda kwa pointi moja mbele ya Alonso akishika nafasi ya pili kwa jumla ya pointi alizokusanya tangu kuanza kwa mashindano ya msimu huu wa 2013/2014 ingawa bado yuko nyuma ya kiongozi wa mashindano na mtetezi wa taji Sebastien Vettel kwa pointi 38.

No comments:

Post a Comment