Sunday, July 28, 2013

WACHEZAJI WAGENI WANAHATARISHA SOKA LA UJERUMANI - BIERHOFF.

MCHEZAJI wa zamani wa kimataifa wa Ujerumani, Oliver Bierhoff anaamini kuwa uchache wa wachezaji katika vilabu vya Bayern Munich na Borussia Dortmund ambao wanacheza katika timu ya taifa ya nchi hiyo unaweza kuwanyima nafasi ya kufanya vizuri katika michuano ya Kombe la Dunia mwakani. Pamoja na mafanikio makubwa ambayo timu hizo mbili imeyapata katika michuano ya Ligi ya Mabingwa barani Ulaya msimu uliopita, Bierhoff ameonyesha wasiwasi wake kwa mwenendo wa timu ya taifa. Badala yake nguli huyo mwenye miaka 45 ametaka hatua za makusudi kwa vilabu vikubwa kuthamini vipaji vya vijana ili kuokoa soka la nchi hiyo lisije kuporomoka. Bierhoff amesema pamoja na Ujerumani kujivunia wachezaji nyota kama Mario Gotze, Mesut Ozil, Thomas Muller na Toni Kroos lakini nchi hiyo bado inakabiliwa na changamoto ya kukosa washambuliaji pamoja na mabeki wa daraja la juu. Nguli huyo amesema kwasasa wanatakiwa kujipanga ili kuhakikisha wanaziba mapengo yaliyopo na kuendelea kubakia katika ushindani.

No comments:

Post a Comment