Sunday, July 28, 2013

SEMENYA ASHINDWA KUFUZU MASHINDANO YA DUNIA.

MWANARIADHA nyota wa kike kutoka Afrika Kusini, Caster Semenya atashindwa kushiriki mashindano ya riadha ya dunia mwezi ujao baada ya kushindwa kufuzu katika mbio za mchujo zilizofanyika nchini Ubelgiji. Semenya alifanikiwa kushinda mbio za mita 800 katika mashindano hayo ya mchujo yaliyofanyika jijini Nivone kwa kutumia muda wa dakika 2 sekunde 01.86 lakini muda huo haukutosha kumfanya kufikia kiwango kilichohitajika ambacho ni dakika 2 sekunde 01.50. Katika mbio hizo Sanne Verstegen wa Uholanzi alimaliza katika nafasi ya pili akitumia muda wa dakika 2 sekunde 02.09. Hiyo ni mara ya kwanza kwa Semenya kushindana toka katika michuano ya olimpiki iliyofanyika jijini London mwaka jana baada ya kipindi kirefu kukaa kando kutokana na maumivu ya goti. 


No comments:

Post a Comment