Thursday, July 25, 2013

POWELL APANIA KUTEREJEA UWANJANI BAADA YA KESI YAKE KUISHA.

MWANARIADHA nyota wa mbio fupi Asafa Powell kutoka Jamaica amesema anataka kurejea uwanjani mapema iwezekanavyo baada ya kushindwa kwenye vipimo vya dawa za kuongeza nguvu. Powell mwenye umri wa miaka 30 alikutwa na chembechembe za dawa ya oxilofrine ambazo zimekatazwa michezoni katika damu yake aliyochukuliwa katika michuano ya riadha ya Jamaica. Mara baada ya taarifa hizo kutoka, Powell alidai kuwa hakutumia dawa hizo kwa makusudi na kwamba atapokea adhabu yoyote itakayotolewa dhidi yake inga wa alikiri kuwa katika kipindi kigumu katika maisha yake ya mchezo huo. Powell na mwanariadha mwingine nyota wa mbio fupi kutoka Marekani Tyson Gay walishinda vipimo hivyo siku 10 zilizopita na sasa wote wanasubiri vipimo vingine ili kuthibitisha kabla ya kutolewa uamuzi wowote dhidi yao. Powell ndio alikuwa mwanariadha wa mwisho kushikilia rekodi ya mbio za mita 100 kabla ya Usain Bolt naye pia wa Jamaica kuja kufunja rekodi hiyo mwaka 2008.

No comments:

Post a Comment