Thursday, July 25, 2013

HIGUAIN, REINA WAFAULU VIPIMO VYA AFYA NAPOLI.

MSHAMBULIAJI wa kimataifa wa Argentina, Gonzalo Higuain na golikipa wa kimataifa wa Hispania Pepe Reina wanakaribia kukamilisha uhamisho wao wa kwenda Napoli baada ya kufaulu vipimo vya afya. Rais wa klabu ya Napoli, Aurelio De Laurentiis aliandika katika ukurasa wake wa mtandao wa kimajii wa twitter kuwa wachezaji hao wawili walifaulu vipimo vyao na wanatarajiwa kujiunga na wenzao muda wowote. Higuain ambaye alikuwa akimendewa na klabu za Arsenal na Juventus, ameripotiwa kuigharimu Napoli euro milioni 37 wakati Reina yeye amejiunga na klabu hiyo kwa mkopo akitokea Liverpool. Mwishoni mwa wiki iliyopita Napoli ilimuuza mshambuliaji wake wa kimataifa wa Uruguay Edinson Cavani kwenda Paris Saint Germain kwa uhamisho ulioweka rekodi wa euro milioni 64.

No comments:

Post a Comment