Thursday, July 25, 2013

SHUTI LA RONALDO LAMVUNJA MKONO MTOTO WA MIAKA 11.

MSHAMBULIAJI nyota wa kimataifa wa Ureno na klabu ya Real Madrid ya Hispania amemvunja mkono mtoto wa miaka 11 kwa bahati mbaya wakati akipiga faulo katika mchezo wa kirafiki dhidi ya timu ya Bournemouth. Mtoto huyo aitwaye Charlie Silverwood alikuwa amekaa nyuma ya goli katika mchezo huo uliochezwa mwihoni mwa wiki iliyopita katika Uwanja wa Goldsands wakati mpira huo uliopigwa na ronaldo ulipomfuata kwa kasi. Akihojiwa Silverwood amesema ilikuwa ni faulo ya kwanza kupigwa na Ronaldo katika mchezo huo na moja kwa moja mpira ulimfuata yeye hivyo alijaribu kuuzuia na kiganja cha mkono wake lakini kutokana na nguvu mpira huo uliusukuma mkono wake juu na kumvunja kiwiko chake. Kijana huyo aliendelea kudai kuwa kuiona Madrid ikicheza na klabu yake ya nyumbani ni bahati ambayo haiji mara mbili hivyo baada ya kuumia aliendelea kumalizia kutazama mchezo huo mpaka mwisho ingawa kwa maumivu na baada ya ndio akaelekea hospitali kupata matibabu. Madrid imemtumia salamu za pole kijana huyo na kumwambia kuwa fulana ya timu hiyo itakayokuwa imesainiwa na Ronaldo itatumwa kwake kama zawadi ya pole.

No comments:

Post a Comment