Saturday, July 27, 2013

WENGER AVUNJA UKIMYA SUALA LA SUAREZ.

MENEJA wa klabu ya Arsenal, Arsene Wenger amevunja ukimya kuhusu klabu hiyo kutaka kumsajili Luis Suarez akidai kuwa klabu hiyo imejiandaa kusubiri ili iweze kupata saini ya mshambuliaji huyo wa Liverpool. Arsenal waliboresha ofa yao kufikia paundi milioni 40 kwa ajili ya mchezaji huyo wa kimataifa wa Uruguay mapema wiki hii lakini mkurugenzi mtendaji wa Liverpool Ian Ayre alithibitisha kuwa ofa zote za klabu hiyo zilikataliwa. Akihojiwa na waandishi wa habari katika ziara yao ya kujiandaa na msimu mpya wa ligi huko jijini Saitama, Japan Wenger amesema kwasasa hawako karibu kumsajili Suarez au mchezaji yoyote yule. Wenger amesema kwasasa ni ngumu kujua mambo yanavyoendelea kwa sababu kila mtu yuko katika ziara hivyo ni ngumu kufanya mawasiliano na watu hivyo baada ya ziara kumalizika anadhani wanaweza kujua kinachoendelea lakini kwasasa inabidi wasubiri.

No comments:

Post a Comment