Saturday, July 27, 2013

LAMOUCHI KUMREJESHA DROGBA.

KOCHA wa timu ya taifa ya Ivory Coast, Sabri Lamouch amesema anatarajia kumtumia nahodha wa timu hiyo Didier Drogba katika mchezo wa kimataifa wa kirafiki dhidi ya Mexico unaotarajiwa kuchezwa Agosti 14 mwaka huu. Mshambuliaji huyo anayekipiga katika klabu ya Galatasaray hajaitumikia timu yake ya taifa toka wapate matokeo mabay katika michuano ya Mataifa ya Afrika iliyofanyika nchini Afrika Kusini mapema mwaka huu. Kocha huyo amekuwa akidai amemuacha Drogba kutokana na kushuka kiwango chake kitu ambacho kimekuwa kikipingwa na mshambuliaji wa zamani wa Chelsea lakini huku akiahidi kuongeza bidii ili kupata tena nafasi katika kikosi hicho. Ivory Coast tayari wamefuzu hatua ya mwisho kwa ajili ya kukata tiketi ya kushiriki michuano ya Kombe la Dunia 2014 na wanatarajia kutumia mechi yao dhidi ya mexico kama maandalizi kwa ajili mchezo wao wa mwisho dhidi ya Morocco. Mchezo huo wa kirafiki dhidi ya Mexico unatarajiwa kufanyika katika Uwanja wa MetLife jijini New York, Marekani.

No comments:

Post a Comment