Saturday, July 27, 2013

MAREKANI YAWANIA TAJI LA TANO MICHUANO CONCACAF.

TIMU ya taifa ya Marekani inatarajiwa kujitupa uwanjani kuwania taji lao la tano la michuano ya Kombe la Dhahabu dhidi ya Panama, michuano ambayo hushirikisha nchi za Amerika kaskazini-CONCACAF. Katika fainali hiyo itakayopigwa baadae leo, Marekani inatarajiwa kuongozwa na mshambuliaji wake nyota Landon Donovan ambaye mpaka sasa amefunga mabao matano katika mechi sita za michuano hiyo alizocheza. Akihojiwa kuhusiana na mchezo huo Donovan amesema kuwa mashindano hayo yamekuwa na mafanikio makubwa kwao na ni mategemeo yao wataendelea kucheza kwa kiwango cha juu na kutawadhwa mabingwa wapya wa michuano hiyo. Marekani inanolewa na Mjerumani Jurgen Klinsmann imewahi kunyakuwa taji hilo mwaka 1991, 2002, 2005 na 2007 huku hii ikiwa ni fainali yake ya tano mfululizo.

No comments:

Post a Comment