Sunday, July 28, 2013

HEYNCKES ASIKITISHWA NA KIPIGO CHA BAYERN.

MENEJA wa zamani wa klabu ya Bayern Munich, Jupp Heynckes amedai kutofurahishwa na matokeo ya timu hiyo kufungwa mabao 4-2 na Borussia Dortmund katika fainali ya Supercup iliyochezwa jana. Heynckes mwenye umri wa miaka 68 ambaye aliiongoza Bayern kushinda mataji matatu msimu uliopita alikuwepo katika Uwanja wa Signal Iduna Park kushuhudia mchezo huo uliokuwa na kila aina ya ushindani. Akihojiwa kocha huyo amesema hana shaka na Pep Guardiola kuipa mafanikio Bayern katika siku zijazo lakini kama ilivyokuwa kwa wengine na yeye pia amesikitishwa na kipigo hicho kwakuwa bado ni vijana wake. Guardiola alichukua nafasi ya Heynckes ambaye mkataba wake ulimalizika msimu uliopita lakini kocha huyo ambaye ni raia wa Ujerumani amesisitiza kuwa hajutii kustaafu. Heynckes amesema kuna mahala mtu unatakiwa kuamua kustaafu na hicho ndicho atakachofanya kwasasa, na kuwa anatizama Bundesliga akiwa ametulia kwenye kochi sebuleni kwake.

No comments:

Post a Comment