Sunday, July 28, 2013

MKONGWE DAVIDS AFANYA KITUKO.

MCHEZAJI wa zamani wa kimataifa wa Uholanzi, Edgar Davids ameamua kufanya kituko kwa kuamua kuvaa fulana yenye namba moja mgongoni msimu huu pamoja na ukweli kwamba yeye ni mchezaji wa kiungo. Davids ambaye ni kocha mchezaji wa klabu ya Barnet amesema ameamua kuvaa fulana yenye namba hiyo ingawa anajua ni utamaduni kwa namba moja kuvaliwa na golikipa. Baada ya namba hiyo kuchukuliwa na Davids sasa golikipa wa Barnet, Graham Stack anatarajiwa kuvaa fulana yenye namba 29 katika msimu mpya ambapo timu hiyo itakuwa ikipambana kujaribu kupanda daraja tena baada ya kushuka msimu uliopita. Stark amesema Davids alimfuata na kumuomba kuvaa fulana yenye namba moja msimu ujao na alimruhusu na kumwambia anaweza kumpa yoyote ile.

No comments:

Post a Comment