Thursday, August 29, 2013

ARSENAL YAMPA FLAMINI MKATABA WA MIAKA MIWILI.

KIUNGO Mathieu Flamini amekuwa mchezaji wa klabu ya Arsenal kwa mara ya pili baada ya kusaini mkataba wa miaka miwili na klabu hiyo jana. Mchezaji huyo wa kimataifa wa Ufaransa alifikia makubaliano na klabu jana ambapo anatarajiwa kulipwa kiasi cha paundi 50,000 kwa wiki huku kukiwa na uwezekano wa kuongezwa mwaka mwingine wa tatu katika mkataba wake. Arsenal inatarajiwa kumtangaza rasmi nyota huyo baada ya kupata ruhusa kutoka kwa viongozi wa Ligi Kuu. Huo unakuwa usajili wa pili kwa Wenger baada ya Yaya Sanogo ambapo wachezaji wote hao walikuwa huru kutokana na kushindwa kuongeza mikataba katika klabu walizokuwepo.

No comments:

Post a Comment