Thursday, August 29, 2013

CHELSEA YAAMUA KUMCHUKUA ETO'O BAADA YA KUCHEMKA KWA ROONEY.

KLABU ya Chelsea inatarajia kumsajili Samuel Eto’o kwa mkataba utakaomuwezesha kukucha kitita cha paundi milioni saba kwa mwaka baada ya kukiri kushindwa kumngo’a Wayne Rooney Manchester United. Eto’o mwenye umri wa miaka 32 atapunguza kiasi kikubwa cha mshahara wake wa paundi milioni 17 kwa mwaka ambao ulikuwa unamfanya kuwa mchezaji anayelipwa zaidi duniani akiwa na klabu ya Anzhi Makhachkala ya Urusi. Hata hivyo kuna ripoti kuwa Anzhi wamemlipa mamilioni ya fedha Eto’o ili kukatisha naye mkataba baada ya klabu hiyo kuamua kupunguza gharama za matumizi na kujaribu kuvuna wachezaji kutoka katika shule yao ya michezo badala ya kununua. Eto’o alitua jijini London kwa treni jana usiku ambapo alipigwa picha akiwa na wakala maarufu Pini Zahavi na anatarajiwa kufanyiwa vipimo vya afya katika uwanja wa mazoezi wa Chelsea kabla ya kumaliza mazungumzo ya mwisho na klabu hiyo.

No comments:

Post a Comment