Thursday, August 29, 2013

MURRAY AANZA VYEMA KUTETEA TAJI LAKE LA US OPEN.

BINGWA mtetezi wa michuano ya wazi ya Marekani, Andy Murray wa Uingereza amefanikiwa kutinga mzunguko wa pili wa michuano kwa kumchapa bila huruma Michael Llodra wa Ufaransa. Murray mwenye umri wa miaka 26 alifanikiwa kushinda kwa 6-2 6-4 6-3 ambapo sasa anatarajiwa kukwaana na Leonardo Mayer wa Argentina katika mzunguko wa pili wa michuano hiyo. Hatua ya kubadilisha mechi ya Murray kuwa mojawapo ya mechi zilizochezwa usiku, hazikuwafurahisha baadhi ya watu ambao wanadhani inaweza kuwa kikwazo kwake huko mbele ukilinganisha na wapinzani wake. Akihojiwa mara baada ya mechi hiyo ambayo ilichezwa jana usiku Murray hakuonyesha kujali muda aliopangiwa kwasababu kuna mechi nyingine pia zilizopangwa muda huo. Kwa upande wa wanawake, mwanadada Venus Williams alijikuta akiiaga michuano hiyo mapema baada ya kukubali kipigo kutoka kwa Zheng Jie wa China kwa 6-3 2-6 7-6. Pamoja na kipigo hicho Williams mwenye umri wa miaka 33 raia wa Marekani alikataa uwezekano wa kustaafu mchezo huo na kudai kuwa bado ataendelea kupambana mpaka dakika za mwisho.

No comments:

Post a Comment