Thursday, August 29, 2013

MARTINO AMZAWADIA VILANOVA TAJI LA SUPERCUP.

MENEJA wa klabu Barcelona, Gerardo Martino amelitoa taji la Supercup walilopata jana kwa kocha wa zamani wa timu hiyo Tito Vilanova ambaye alilazimika kubwaga manyanga kutokana na kusumbuliwa na saratani ya koo. Barcelona walilazimishwa sare ya bila ya kufungana nyumbani dhidi ya Atletico jana hivyo kutawadhwa mabingwa wa Supercup baada ya kushinda kwa bao la ugenini walilopata katika sare ya bao 1-1 waliyopata katika mechi ya mkondo wa kwanza. Akizungumza na waandishi wa habari, Martino amesema fainali hiyo ilikwenda vyema kutokana na kazi nzuri iliyofanywa msimu uliopita hivyi wamekuwa mabingwa kwasababu ya wacheza, Vilanova na benchi lake lote la ufundi. Katika mechi hiyo Lionel Messi na Neymar walioanza katika kikosi cha kwanza cha Barcelona kwa mara ya kwanza na Martino anaamini kuwa wawili hao wataelewana vizuri zaidi katika siku za usoni. Martino alikiri wawili hao kutoelewana vizuri katika mechi hiyo lakini hana shaka kwamba katika siku zijazo watacheza vyema kwa pamoja na kutengeneza safu hatari ya ushambuliaji.

No comments:

Post a Comment