Thursday, August 29, 2013

BOLT ATAMBA KUSHINDA ZURICH.

MWANARIADHA nyota wa mbio fupi, Usain Bolt wa Jamaica amesema amepumzika na yuko tayari kukimbia muda mwingine wa haraka wakati atakaposhindana katika mashindano ya Diamond League jijini Zurich, Switzerland. Bolt alishinda medali tatu katika mashindano ya Dunia yaliyofanyika jijini Moscow mapema mwezi huu huku akishinda mbio za mita 100 kwa kutumia muda wa sekunde 9.77. Akihojiwa kabla ya mbio hizo zinazotarajiwa kufanyika kesho, Bolt amedai kupata mapumziko ya kutosha hivyo anaamini anaweza kukimbia chini ya sekunde 9.80 katika Uwanja wa Letzigrund. Bolt ambaye alishinda mbio za mita 200 kwa kutumia sekunde 19.66 katika uwanj huohuo mwaka jana, atachuana na Justin Gatlin wa Marekani na Mjamaica mwezake Nesta Carter ambao walishinda medali za fedha na shaba katika mashinano ya dunia.

No comments:

Post a Comment