Sunday, August 25, 2013

BALE ATUA HISPANIA KUMALIZIA UHAMISHO WAKE KWENDA MADRID.

MSHAMBULIAJI nyota wa klabu ya Tottenham Hotspurs, Gareth Bale ametua nchini Hispania kujiandaa kuweka saini Real Madrid lakini klabu hizo mbili bado zinavutana kuhusiana na rekodi ya usajili kwenye uhamisho huo. Nyota huyo wa kimataifa wa Wales mwenye umri wa miaka 24 alitua Malaga kwa ndege binasfi na kwenda kwa teksi hadi Marbella, ambako anatarajiwa kukaa kwa ajili ya kukamilisha majadiliano ya dakika za mwisho kabla ya kufungwa kwa pazia la usajili. Inafahamika kuwa Madrid imetenga kitita cha euro milioni 100 sawa na paundi milioni 86 ikijumuisha na malipo kadhaa ndani ya miaka mitatu au minne, baada ya paundi milioni 70 kulipwa taslimu.  Real Madrid inacheza na Granada Jumatatu usiku katika La Liga na kama kutambulishwa kwa Bale itakuwa Jumanne. Bale, ambaye alijiunga na Spurs kwa dau la paundi milioni 10 kutoka Southampton mwaka 2007, alishinda tuzo ya Mwanasoka Bora wa Mwaka wa Chama cha Wachezaji wa Kulipwa na Waandishi wa Soka msimu uliopita, ameifungia mabao 26 Spurs.

No comments:

Post a Comment