Saturday, August 24, 2013

CASILLAS ANAPASWA KUFIKIRIA KWENDA BARCELONA - CANIZARES.

GOLIKIPA wa zamani wa klabu ya Real Madrid, Santiago Canizares amedai kuwa Iker Casillas anapaswa kufikiria kuondoka katika klabu hiyo na kwenda Barcelona. Casillas ambaye ni nahodha wa Madrid alijikuta akipoteza nafasi ya kipa namba moja kwa Diego Lopez msimu uliopita wakati Jose Mourinho akiwa hapo na pia ameonekana kubakia kuwa chaguo la pili hata chini ya kocha mpya Carlo Ancelotti. Kutokana na suala hilo Canizares haoni sababu ya Casillas kushindwa kwenda Barcelona ambako anaweza kujihakikishia kucheza katika kikosi cha kwanza. Canizares amesema kwa jinsi mambo yanavyokwenda hapo Madrid ni wazi kwamba Casillas atakuwa hana chake hivyo huu ni wakati wa kufikiria kwenda kuanza kwingine. Casillas kwasasa ana mkataba na Madrid ambao unamalizika mwaka 2017.

No comments:

Post a Comment