Saturday, August 24, 2013

SINA UHAKIKA WA KIKOSI CHA KWANZA - TERRY.

NAHODHA wa klabu ya Chelsea, John Terry amesisitiza kuwa hajahakikishiwa nafasi ya kuanza katika kikosi cha kwanza cha timu hiyo na Jose Mourinho msimu huu. Terry alijikuta mara kwa mara akikosa namba katika kikosi cha Chelsea kilichokuwa kikinolewa na Rafael Benitez kutokana na kuandamwa na majeruhi ya mara kwa mara msimu uliopita. Lakini Mourinho amempa nafasi beki huyo mkongwe kucheza dakika zote 90 katika mechi ya ufunguzi wa Ligi Kuu nchini Uingereza lakini Terry mwenyewe anajua kuwa bado ana kazi kubwa ya kufanya ili kuhakikisha anapata nafasi ya kidumu kwenye kikosi cha kwanza. Terry amesema hata kama ukiwa nahodha haimaanishi kuwa ndio utakuwa na nafasi ya kudumu katika kikosi cha kwanza na Mourinho mwenyewe aliweka wazi toka siku ya kwanza aliyotua Stamford Bridge kwa mara ya pili. Chelsea inatarajiwa kuchuana na Manchester United Jumatatu usiku, klabu ambazo zinapewa nafasi ya kuchuana katika kugombea taji la ligi la nchi hiyo msimu huu.

No comments:

Post a Comment