Saturday, August 24, 2013

WACHEZAJI WATATU WA MALAWI WAFARIKI KWA AJALI.

SOKA nchini Malawi limekumbwa na simanzi kubwa baada ya wachezaji watatu wa timu ya Mafco kufariki katika ajali ya gari iliyotokea Ijumaa asubuhi katika mji wa Nkhotakota. Wachezaji hao Sadani Magwere, Gift Mphonde na Chifundo Phiri walifariki katika eneo la tukio baada ya gari la jeshi walilokuwa wakisafiria kutoka katika mechi ya robo fainali ya Kombe la Carlsberg kupata ajali. Polisi walithibitisha kuwa wachezaji wengine watatu Sailesi Phiri, Jimmy Mzunga na Gift Soko wamelazwa hospitalini wakiuguza majeraha ya ajali hiyo. Katika taarifa yake Mwenyekiti wa Mafco, Chitumbo Charamba aliwaambia wanahabari kuwa mwili wa Phiri unatarajiwa kuzikwa wilaya ya Kasungu wakati wengine wawili wao wazikwa katika mji mkuu wa zamani wa Zomba leo.

No comments:

Post a Comment