Saturday, August 24, 2013

MADRID KUFANYA ZIARA ALGERIA MWAKANI.

KLABU ya Real Madrid ya Hispania, imethibitisha kufanya ziara nchini Algeria mwakani ambapo watacheza mechi ya kirafiki na mojawapo ya vilabu vya huko. Awali ziara ya Madrid chini humo ilitakiwa kufanyika mwishoni mwa msimu huu lakini ilishindakana kwasababu ya kuingiliana na mwezi mtukufu wa Ramadan hivyo baadhi ya maandalizi ya mwiho kushindwa kukamilika. Kwa mujibu wa waratibu wa ziara hiyo kampuni za Mobilis na Mediapro za huko, mkataba wa makubaliano tayari umesainiwa na tarehe kwa ajili ya tukio hilo inatarajiwa kutajwa wakati wowote. Waratibu hao wamesema klabu ambayo itacheza na Madrid wakati wa ziara hiyo nchini Algeria itachaguliwa na mashabiki watakaopiga kura katika mtandao.

No comments:

Post a Comment